Tuesday, December 23, 2014

YAH: MZUNGUKO WA PILI LIGI YA MKOA (AZAM BD LEAGUE) 2015

Chama cha Mpira wa kikapu Mkoa wa Dar Es Salaam kinapenda kuwajulisha wadau wake wote kuwa mzunguko wa pili wa ligi tajwa unatarajiwa kuanza tarehe 9 January 2015 na kumalizika 14 March 2015 baada ya mapumziko yaliyopisha mashindano ya vyuo (SHIMIVUTA) yaliyo malizika hivi karibuni mkoani Tanga na Sherehe za Xmas na Mwaka Mpya. Hivyo basi michezo ya ligi itachezwa siku za Ijumaa Jioni,Jumamosi na Jumapili chini ya udhamini wa Bakhresa Food...

Monday, December 1, 2014

Temeke Mabingwa - Taifa Cup 2014 Dodoma

Timu pekee ya Temeke kutokea Mkoa wa Dar Es Salaam imefanikiwa kutwaa taji la Taifa Cup 2014 kwenye michuano iliyofanyika Mkoani Dodoma baada ya kuifunga Timu ngumu ya Mkoa wa Mbeya kwa jumla ya vikapu 85 - 43. ...

AZAM BD LEAGUE - KUKAMILISHA MECHI ZA VIPORO

Chama cha Mpira wa Kikapu Mkoa wa Dar Es Salaam kinapenda kutoa taarifa kwa vilabu vya JOGOO,DB Young Stars,Kurasini Heats,DB Lioness,Mgulani na Jeshi Stars kuwa michezo yao ya viporo itafanyika tarehe 5 na 6 Desemba 2014 hii inatokana na matumizi ya uwanja kuwa na shughuli za michezo ya Ngumi za Kimataifa. Tafadahali barua husika za taarifa hii zitawafikia vilabuni kwenu. ...